CLICK HAPA

Friday, June 15, 2012

BAJETI NI BALAA AU NI TUNU

   Watanzania wapo katika sintofahamu wakijiuliza maswali mengi kama bajeti itakuwa ni Balaa au tunu? Hali hii, inatokana na ukweli kwamba bajeti ya mwaka 2011/2012, imemalizika, huku kukiwa na utekelezaji duni katika baadhi ya maeneo.

Kwa mfano wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, iliongezewa fedha katika sekta ya usafiri wa meli, ambapo ilitengewa Sh bilioni 9, lakini hadi mwaka unamalizika Serikali ilikuwa haijapeleka fedha ilizoahidi katika bajeti hiyo. Akiwasilisha mwelekeo wa bajeti ya 2012/13 mbele ya Kamati ya Fedha na Uchumi, Dar es Salaam wiki iliyopita, Waziri wa Fedha, Dk Mgimwa, alisema inatarajiwa kuwa Sh trilioni 15, ikilinganishwa na Sh trilioni 13.5 za mwaka 2011/12.
Alisema bajeti hiyo, imeweka vipaumbele saba, kipaumbele cha kwanza kikiwa ni miundombinu.Miundombinu imegawanyika katika makundi manne ya reli, umeme, maji salama, usafirishaji na uchukuzi ambavyo vimetengewa Sh trilioni 4.5. Vipaumbele vingine katika bajeti hiyo ni kilimo, viwanda, rasilimali watu, huduma za jamii, utalii, biashara ya ndani na nje na huduma za fedhaHata hivyo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa fedha zilizopelekwa katika Wizara ya Uchukuzi kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Sh bilioni 252, huku sekta ya usafiri wa reli ikitengewa matumizi ya Sh bilioni 130.

UKUBWA WA PUA SI WINGI WA MAKAMASI


PAMOJA KIFARU (RHINO) NA UKUBWA WAKE WOTE NA UKALI WAKE ANAMWOGOPA MTOTO WA MBWA. HUWEZI AMINI LAKINI NDIO ILIVYO. WAHENGA WALISEMA UKUBWA WA PUA SI WINGI WA MAKAMASI.  INAWEZEKANAJE  MNYAMA  MKUBWA KAMA KIFARU KUMWOGOPA MBWA WALA SI MBWA KAMILI BALI KITOTO CHA MBWA NI JAMBO LA KUSHANGAZA NA KUSTHAJABISHA NILILOSHUHUDIA NI SAWA NA LEO KUKUTA MTU MZIMA NA NDEVU ZAKE  ANAOGOBA SISIMIZI. 

Thursday, June 14, 2012

EURO 2012 YAENDELEZA VISASI VYA VITA VYA PILI VYA DUNIA

Polisi imewatia mbaroni watu 184,ikiwa ni raia 156 wa Poland na Warussi 24 kufuatia mapigano makali baina ya mashabiki ambao waliwashambulia Polisi pia.
Wakuu wa nchi walikua wamejiandaa kwa uwezekano wa mtafaruku kutokea kabla ya mchuano wa jumanne ikizingatiwa kwamba uhusiano kati ya nchi hizi mbili umetiwa sumu na migogoro ya miaka mingi ikikumbukwa pia uvamizi na utekaji wa Poland kwa kipindi cha miaka 40 baada ya vita vikuu vya pili vya Dunia.
Ghasia zilizuka wakati maelfu ya mashabiki wa Urussi wakisindikizwa na polisi walivuka mto Vistula wakiwa njiani kwenda uwanjani. Mapigano mengine yalizuka katikati ya mji katika eneo la mashabiki baada ya mechi iliyomalizika kwa sare ya bao moja kwa kila upande.
 Waliopigana wakamatwa
Waliokamatwa watahukumiwa na mamlaka inayohusika.





Mbali na matukio ya nje ya uwanja, mechi iliendelea bila tatizo ndanio ya uwanja bila kubaguana. Kinyume na ilivyo katika mechi za Ligi nyingi barani Ulaya safari hii hapakuepo wasimamizi kulinda usalama kwa kusimama katikati ya makundi ya mashabiki wanaokinzana.

Wednesday, June 13, 2012

TANZANIA YAFANIKIWA KUMKAMATA GAIDI ERDOGAN

      MOJA YA MILIPUKO ERDOGAN ANASADIKIWA KUSHIRIKI JIJINI NAIROBI-KENYA
Polisi ya Kenya inasema kuwa Emrah Erdogan ni raia wa Ujerumani mwenye asili ya Uturuki.
Kenya inadai kuwa alivuka mpaka mapema mwezi Mayi kutoka Somalia ambako alishiriki mapigano kwa niaba ya kundi la Al Shabab.
Zaidi ya watu 30 walijeruhiwa katika mlipuko ambao wakuu wa Kenya wanasema ulisababishwa na bomu hilo.Kumekuepo na sintofahamu juu ya chanzo cha mlipuko huo- ambapo Maofisa wa Polisi walianza kwa kusema kuwa mlipuko huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme.
Mara kwa mara kundi la Al Shabab limetishia kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi nchini Kenya kwa sababu nchi hio ilituma vikosi nchini Somalia.
Serikali ya Kenya inalituhumu kundi la wapiganaji wa Al Shabab kuhusiana na utekaji nyara wa watu kadhaa kwenye ardhi yake pamoja na kusababisha hali ya wasiwasi kwenye mpaka baina yake na Somalia.
EMRAH  ERDOGAN
Polisi ya Tanzania imethibitisha kuwa Erdogan alikamatwa na kuahidi maelezo zaidi baada ya kumuhoji.
Erdogan ni miongoni mwa watu wanne ambao Polisi ya Kenya imekua ikiwasaka tangu kutokea kwa mlipuko huo.
Ilisambaza picha yake na kuomba habari kuhusu mahali alipo.
Erdogan, anayejulikana pia kama Salahuddin al-Kurdi, inaaminika kuwa aliwahi kusafiri kwenda Waziristan huko Pakistan ya kaskazini magharibi mwaka 2010 ambako alijiunga na kundi la wakereketwa wenye imani kali kabla ya kuelekea Somalia mwaka jana, kwa mujibu wa shirika la habari Reuters.
Mapema mwaka huu, vikosi vya AU vinavyounga mkono serikali ya mseto nchini Somalia viliongezea idadi ya askari wake kutoka 12,000 hadi 18,000 kujumuisha vikosi vya Kenya vilivyoingia nchi hio mnamo mwezi Oktoba mwaka jana kuwasaka wapiganaji wa Al Shabab.
Kundi la Al-Shabab, lililojiunga na mtandao wa al-Qaeda mapema mwaka huu imefahamika lilisajili wapiganaji wa kigeni kadhaa -wengi ambao wamewahi kupigana huko Iraq na Afghanistan                                                

Tuesday, June 12, 2012

EURO 2012 - RACISM


Media reports suggested that Italy striker Mario Balotelli was subjected to racist chanting during the match with Spain in Gdansk on Sunday.

Two days previously, Czech Republic full-back Theodor Gebre Selassie revealed he had 'noticed' racist chants directed at him during the game against Russia in Wroclaw.

No official complaint has been made to UEFA by either the Italy or Czech Republic football associations.

However, subsequent information has prompted UEFA to launch a formal investigation into both incidents.
Following the provision of new independent information today, regarding the two cases of alleged racist chanting in the Spain-Italy and Russia-Czech Republic matches, UEFA is now conducting further investigations, read a UEFA statement.
No disciplinary proceedings
There are, however, no disciplinary proceedings opened at this moment in time.

Meanwhile, UEFA has confirmed disciplinary proceedings have been opened against the Croatian Football Association for the behaviour of their fans against Ireland on Sunday.
Supporters celebrated their second goal by letting off flares and firecrackers while a fan in a Croatia shirt ran onto the pitch in order to celebrate with national team coach Slaven Bilic. UEFA confirmed Croatia have been charged with the setting off and throwing of fireworks and missiles, and the invasion of the pitch.


Sunday, June 10, 2012

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI AFARIKI

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI KENYA GEORGE SAITOTI AKIWA NA MSAIDIZI WAKE ORWA  OJODE WAMEPATA AJALI WAKIWA KWENYE AJALI YA HELKOPTA MAENEO NGONG NA KUFARIKI HAPO HAPO. MWENYEZI MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU  HAWA MAHALI PEMA PEPON. AMEN
  WAZIRI WA MAMBO YA NDANI KENYA GEORGE SAITOTI ENZI ZA UHAI WAKE
 NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI KENYA ORWA OJADE

Abiria wote sita, wakiwemo marubani wawili na walinzi wa mawaziri hao waliokuwa kwenye helikopta hiyo wamefariki dunia na miili yao kuteketezwa kwa kiasi cha kutoweza kutambulika.
Kilichosababisha ajali hiyo bado hakijabainika.
Bwana Saitoti na maafisa wengine wa juu katika wizara ya usalama wa ndani walikuwa wakielekea katika eneo la Sotik kwa mkutano wa usalama. Saitoti alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Kenya waliokuwa wakipania kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Walioshuhudia ajali hiyo wamesema waliona helikota hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika msitu wa Ngong.
Polisi wamezingira eneo la ajali hiyo na kamishna wa polisi Mathew Iteere aliyepo katika eneo la ajali anatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusiana na ajali hiyo.
Ajali hiyo ya helikopta imetokea katika siku ambapo Kenya inaadhimisha miaka minne tangu kutokea ajali ya ndege iliyowauwa mawaziri wengine wa serikali, Kipkalya Kones na Lorna Laboso.

Miili ya marehemu imeungua vibaya na moto hivyo utambuzi wa miili hiyo utakuwa mgumu.Mkuu wa polisi aelekea eneo la tukio.Chanzo cha ajali hiyo mbaya bado hakijajulikana.Tetesi zimeshaanza kuhusisha ajali hii na kikundi cha ugaidi cha Al Shabab cha nchini Somalia pamoja na mbio za urais nchini Kenya.RI.P marehemu wote.

BOB MAKANI MUASISI WA CHADEMA AMEFARIKI

BOB MAKNI KADA NA MUASISI  WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO CHADEMA AFARIKI. BOB MAKANI ALIKUA MWENYEKITI WA CHADEMA KABLA YA MBOWE. PIA BOB MAKANI ALISHAKUWA MSAIDIZI WA GAVANA BENKI KUU YA TANZANIA. MWENYEZI MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI.
 HISTORIA YAKE CDM-Katibu Makuu wa kwanza wa CHADEMA kati ya mwaka 1993 hadi 1998, Mwenyekiti wa CHADEMA kuanzia mwaka 1998 hadi 2004 na mgombea ubunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kati ya mwaka 1995.
border: 0" />

Translate