CLICK HAPA

Friday, July 13, 2012

MADAKTARI WANATAKA KUANDAMANA

KITENDO cha Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT), kusitisha usajili kwa baadhi ya madaktari waliokuwa kwenye mafunzo ya vitendo (Interns), kimekoleza moto wa mgomo wa madaktari baada  ya wanataaluma hao kutangaza maandamano yatakayofanyika wakati wowote kuanzia sasa.

Kwa muda wa wiki tatu sasa, madaktari wamekuwa katika mgomo wakitaka kuboreshewa masilahi yao na huduma za afya hospitalini, lakini wanataaluma hao walionekana kuchukizwa zaidi baada ya tukio la kutekwa, kupigwa na kutelekezwa porini kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka huku rais wa Chama cha Madaktari (MAT), Dk Namala Mkopi akifunguliwa mashtaka ya kukiuka amri ya mahakama.    

Jana, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa MAT, Dk Rodrick Kabangila alitaja lengo la maandamano hayo kuwa ni kupinga dhuluma na uonevu dhidi ya taaluma ya udaktari  na madaktari wenyewe.

Dk Kabangila alitaja sababu ya pili kwamba, ni kulaani kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka cha kutekwa, kupigwa, kuteswa na kutupwa katika msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na sababu ya tatu ni  kushinikiza Serikali kuunda Tume  Huru ya kuchunguza suala hilo, ili wahusika wajulikane na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema pia kwamba hatua hiyo imekuja kutokana na kitendo cha Serikali kuendelea kuchukua hatua ya kuwafukuza madaktari na kusitishiwa leseni wale waliokuwa chini ya mafunzo, badala ya kusikiliza na kutatua madai yao yaliyolenga kuboresha huduma hiyo nchini.

“Kama mnavyofahamu, mpaka sasa takriban madaktari 400 walio chini ya usimamizi na wale walio kazini wamesitishiwa usajili na wengine kusimamishwa kazi, na haya yanaendelea wakati suala la msingi likiwa mahakamani na pia Tanzania ikiwa na upungufu mkubwa wa madaktari kwa daktari mmoja kuwa na uwiano wa kuhudumia wagonjwa 30,000,” alisema Dk Kabangila na kuongeza:

“MAT inasikitishwa na dhuluma hii inayoendelea dhidi ya taaluma ya udaktari na madaktari wenyewe na hivyo inapanga kuitisha mkutano mkubwa kesho (leo) na inatangaza maandamano ya amani ya madaktari na wale wote wenye mapenzi mema na taaluma hii na sekta ya afya kwa ujumla.”

Dk Kabangila aliongeza kuwa, maandamano hayo yatafuata taratibu zote za kisheria, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa polisi saa 48 kabla ya kuandamana na madaktari wote watavaa makoti meupe na wasio madaktari watatakiwa kuwa na vitambaa vyeupe.

Alisema maandamano hayo ya amani yataanzia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) hadi Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ambako watakabidhi madai yao serikalini.

“Tunajua tunachotakiwa kufanya ni kutoa taarifa kwa ajili ya kuhitaji ulinzi. Maandamano yetu ni ya amani na ndiyo sababu tutakuwa na makoti pamoja na vitambaa vyeupe kwa wasio madaktari, ”alisisitiza.

Katika mkutano huo, Dk Kabangila alielezea kusikitishwa kwake na makundi ya watu mbalimbali na mtu mmoja, mmoja kuwatuhumu kuwa ni wauaji kwa kuendesha mgomo, akisema kitendo hicho ni hatari kwa kuwa kinawakatisha tamaa  madaktari nchini.

“Yameibuka makundi yanayowatuhumu madaktari kupitia vyombo vya habari, wapo wanaosema madaktari ni wauaji, hii ni hatari. Madaktari wanafanya kazi ngumu na katika mazingira magumu, hawana vitendea kazi lakini badala ya kuwafariji, watu wanajitokeza na kuwasema vibaya, sijui nini malengo yao na hatima ya taaluma ya udaktari nchini,” alisema.

Alisema lengo la kushinikiza madai yao ni kutaka Serikali iweke mazingira mazuri yatakayowezesha wanataalamu hao ambao Serikali hutumia fedha nyingi kuwasomesha, kufanya kazi nchini badala ya kukimbilia nje ya nchi.

Tuesday, July 10, 2012

MGOMO WA MABASI MOSHI UNAENDELEA

PILIKAPILIKA NDANI YA MJI WA MOSHI JANA ZILIKWAMA BAADA YA MABASI YOTE YA NAYOTOA HUDUMU YA USAFIRISHAJI WA NDANI YA MKOA KUGOMA KUTOKANA NA KUPANDISHIWA ADA YA USHURU. MADEREVA WA MABASI HAYA WALIKATAA ULIPA USHURU WA SHILINGI 1500 WAKIDAI WANATAKA KULIPA SHILINGI 500.

      MAMIA YA ABIRIA WALIKUA WAMEKWAMA KUSAFIRI STENDI YA KUU YA MOSHI MJINI 
border: 0" />

Translate